MCHEZAJI namba moja Duniani katika mchezo wa tenisi, anayefahamika kwa jina la Asheleigh Barty, ameshangaza ulimwengu wa mchezo huo, kwa kutangaza kuwa atastaafu kucheza tenisi akiwa na umri wa miaka 25 pekee. Inaripoti BBC … (endelea).
Raia huyo wa Australia alitoa tangazo hilo, kwenye mitandao ya kijamii siku ya jumatano, akisema kuwa anaondoka ili kufuata ndoto zingine.
Amesema ‘’Nina furaha sana na niko tayari na ninajua kwasasa moyoni mwangu nina furaha ‘’ alisema kwenye video.
Hata hivyo, Barty alishinda Grand Slam yake ya kwanza kwenye French Open mwaka 2019.
Pia amebaki kuwa mchezaji wa nafasi ya juu tangu wakati huo, akiungwa mkono na mafanikio katika Wimbledon mwaka jana 2021.
Aidha mnamo Januari alikuwa mchezaji wa kwanza wa nyumbani, kushinda taji la Australia Open la wanaume na wanawake katika kipindi cha miaka 44.
Leave a comment