Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Majeshi Urusi yateka mitambo ya nyuklia Ukreini, mataifa yaonya
Kimataifa

Majeshi Urusi yateka mitambo ya nyuklia Ukreini, mataifa yaonya

Spread the love

 

UKREINI imesema majeshi ya Urusi yameshambulia na kuteka mtambo wa kuzalisha nishati ya nyuklia wa Zaporizhzhia ambao ni mkubwa zaidi barani Ulaya. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

“Wasimamizi wanaendelea kufuatilia hali ya uzalishaji wa nishati,” zimesema mamlaka za mitaa katika mitandao ya kijamii na kunukuliwa na shirika la habari la Reuters.

Imeripotiwa kuwa mapema leo moto mkubwa ulilipuka katika mitambo hiyo kufuatia mashambulizi ya makombora ya Urusi.

Kikosi cha kutoa huduma ya dharura kilifanikiwa kuuzima moto huo ambao uliwaka nje ya jengo lililopo eneo la mtambo.

Viongozi wa dunia wameishutumu Urusi kwa kujaribu kuhatarisha bara zima la Ulaya kwa kushambulia mitambo hiyo.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema mashambulizi ya “kizembe” ya Urusi yanahatarisha usalama wa bara zima la Ulaya.

Naye Rais wa Marekani, Joe Biden ameitaka Moscow kusitisha shughuli za kijeshi karibu na eneo hilo wakati Waziri Mkuu wa Canada, Justine Trudeau amesema “mashambulizi ya kuogofya” kutoka Urusi “lazima yasitishwe mara moja”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!