UKREINI imesema majeshi ya Urusi yameshambulia na kuteka mtambo wa kuzalisha nishati ya nyuklia wa Zaporizhzhia ambao ni mkubwa zaidi barani Ulaya. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
“Wasimamizi wanaendelea kufuatilia hali ya uzalishaji wa nishati,” zimesema mamlaka za mitaa katika mitandao ya kijamii na kunukuliwa na shirika la habari la Reuters.
Imeripotiwa kuwa mapema leo moto mkubwa ulilipuka katika mitambo hiyo kufuatia mashambulizi ya makombora ya Urusi.
Kikosi cha kutoa huduma ya dharura kilifanikiwa kuuzima moto huo ambao uliwaka nje ya jengo lililopo eneo la mtambo.
Viongozi wa dunia wameishutumu Urusi kwa kujaribu kuhatarisha bara zima la Ulaya kwa kushambulia mitambo hiyo.
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema mashambulizi ya “kizembe” ya Urusi yanahatarisha usalama wa bara zima la Ulaya.
Naye Rais wa Marekani, Joe Biden ameitaka Moscow kusitisha shughuli za kijeshi karibu na eneo hilo wakati Waziri Mkuu wa Canada, Justine Trudeau amesema “mashambulizi ya kuogofya” kutoka Urusi “lazima yasitishwe mara moja”
Leave a comment