Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Majeshi Urusi yateka mitambo ya nyuklia Ukreini, mataifa yaonya
Kimataifa

Majeshi Urusi yateka mitambo ya nyuklia Ukreini, mataifa yaonya

Spread the love

 

UKREINI imesema majeshi ya Urusi yameshambulia na kuteka mtambo wa kuzalisha nishati ya nyuklia wa Zaporizhzhia ambao ni mkubwa zaidi barani Ulaya. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

“Wasimamizi wanaendelea kufuatilia hali ya uzalishaji wa nishati,” zimesema mamlaka za mitaa katika mitandao ya kijamii na kunukuliwa na shirika la habari la Reuters.

Imeripotiwa kuwa mapema leo moto mkubwa ulilipuka katika mitambo hiyo kufuatia mashambulizi ya makombora ya Urusi.

Kikosi cha kutoa huduma ya dharura kilifanikiwa kuuzima moto huo ambao uliwaka nje ya jengo lililopo eneo la mtambo.

Viongozi wa dunia wameishutumu Urusi kwa kujaribu kuhatarisha bara zima la Ulaya kwa kushambulia mitambo hiyo.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema mashambulizi ya “kizembe” ya Urusi yanahatarisha usalama wa bara zima la Ulaya.

Naye Rais wa Marekani, Joe Biden ameitaka Moscow kusitisha shughuli za kijeshi karibu na eneo hilo wakati Waziri Mkuu wa Canada, Justine Trudeau amesema “mashambulizi ya kuogofya” kutoka Urusi “lazima yasitishwe mara moja”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!