Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Putin kuburuzwa Mahakama ya kimataifa (ICC)
Kimataifa

Putin kuburuzwa Mahakama ya kimataifa (ICC)

Spread the love

 

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Uhalifu ICC inatarajia kuanza uchunguzi kuhusu uwezekano wa uhalifu wa kivita nchini Ukraine hali ambayo inatafsiriwa kumweka matatani Rais wa Urusi, Vladimir Putin. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya jana tarehe 1 Machi, 2022 Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC, Karim Khan kusema kuwa mahakama hiyo itaanzisha uchunguzi kuhusu uwezekano wa uhalifu wa kivita unaofanywa na Urusi nchini Ukraine.

Katika taarifa, Khan amesema maamuzi ya uchunguzi kuhusiana na hali nchini Ukraine haraka yataanza haraka iwezekanavyo.

Khan amesema baada ya kupitia uchunguzi wa awali wa hali hiyo, ameridhika kwamba kuna sababu za kimsingi za kuamini kwamba madai yote ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu vimefanyika nchini Ukraine katika matukio kabla ya uvamizi wa Urusi.

Khan ameongeza kuwa kwa kuzingatia kupanuka kwa mzozo huo katika siku za hivi karibuni, ni nia yake kwamba uchunguzi huo pia utajumuisha madai yoyote mapya ya uhalifu yaliyo chini ya mamlaka ya ofisi yake ambayo yatafanywa na pande yoyote katika mzozo huo katika eneo lolote la Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!