Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Burkina Faso awekwa kizuizini
Kimataifa

Rais Burkina Faso awekwa kizuizini

Spread the love

Rais wa Burkina Faso, Roch Marc Christian Kaboré amezuiliwa katika kambi ya jeshi nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Reuters ni kwamba milio ya risasi ilisikika jana jioni tarehe 23 Januari, 2022 karibu na makazi ya rais wa Burkina Faso.

Inaelezwa kuwa hayo yamejiri baada ya wanajeshi kuasi katika kambi kadhaa wakidai kuondolewa kwa viongozi wakuu wa kijeshi na kuwezeshwa zaidi katika mapambano dhidi ya waasi wa Kiislamu.

Hata hivyo, serikali imekanusha uvumi juu ya mapinduzi hayo

Waandamanaji wanaopinga namna serikali inavyoshughulikia uasi wa wafuasi wa itikadi kali, waliyachoma moto makao makuu ya chama tawala mjini Ougadougou.

Siku ya Jumamosi, wanajeshi wasiopungua wawili waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mlipuko wa bomu lililotengenezwa kienyeji, kwenye barabara kati ya Ouahigouya na Titao (Kaskazini).

Mlipuko huo ulitokea wakati gari lao lililokuwa likiwasindikiza wafanyabiashara lilipokanya bomu hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!