Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Burkina Faso awekwa kizuizini
Kimataifa

Rais Burkina Faso awekwa kizuizini

Spread the love

Rais wa Burkina Faso, Roch Marc Christian Kaboré amezuiliwa katika kambi ya jeshi nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Reuters ni kwamba milio ya risasi ilisikika jana jioni tarehe 23 Januari, 2022 karibu na makazi ya rais wa Burkina Faso.

Inaelezwa kuwa hayo yamejiri baada ya wanajeshi kuasi katika kambi kadhaa wakidai kuondolewa kwa viongozi wakuu wa kijeshi na kuwezeshwa zaidi katika mapambano dhidi ya waasi wa Kiislamu.

Hata hivyo, serikali imekanusha uvumi juu ya mapinduzi hayo

Waandamanaji wanaopinga namna serikali inavyoshughulikia uasi wa wafuasi wa itikadi kali, waliyachoma moto makao makuu ya chama tawala mjini Ougadougou.

Siku ya Jumamosi, wanajeshi wasiopungua wawili waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mlipuko wa bomu lililotengenezwa kienyeji, kwenye barabara kati ya Ouahigouya na Titao (Kaskazini).

Mlipuko huo ulitokea wakati gari lao lililokuwa likiwasindikiza wafanyabiashara lilipokanya bomu hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!