Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Guardiola, Trend watamba tuzo mwezi Novemba Epl
Michezo

Guardiola, Trend watamba tuzo mwezi Novemba Epl

Pep Guardiolla
Spread the love

 

Kocha wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi Novemba kwenye Ligi Kuu nchini England “EPL”,. Huku beki wa kulia wa klabu ya LiverPool Trend Alexander Arnold akichagulia kama mchezaji bowa wa Ligi hiyo kwa mwezi Novemba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Ndani ya mwezi Novemba Beki huyo wa kulia wa Liverpool amecheza michezo mitatu, huku akifunga bao moja na kutoa pasi za mabao (assist) nne, katika mabao 10 yaliyofungwa na timu hiyo katika michezo hiyo mitatu.

Katika kinyang’anyiro hiko mchezaji huyo alikuwa akichuanao na Joao Cancelo na Bernardo Silva wote kutoka Manchester City, Diogo Jota kutoka Liverpool, Emmanuel Dennis Watford, na John McGinn wa Aston Villa.

Kwa upande wa Guardiola, katika mwezi Novemba amefanikiwa kuiongoza Manchester City kwenye michezo mitatu na kushinda yote na hivyo kutwaa tuzo hii kwa mara ya 10 toka alipojiunga na klabu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!