Friday , 26 April 2024
Michezo

Spread the love

Simba waigomea TFF

KATIKA hali ya kushangaza uongozi wa klabu ya Simba ulimzuia kocha wake mkuu Pablo Franco Martin kutoongea na waandishi wa Habari, kufuatia uwepo wa bango lenye lenye nembo ya kampuni ya Gsm ambao ni sehemu ya udhamini wa Ligi hiyo kufuatia klabu hiyo kutotambua mkataba huo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mkutano huo dhidi ya waandishi wa habari ambao huko kikanuni ambao unatakiwa kufanyika siku moja kabla ya mchezo kwa makocha wa timu zote mbili kuzungumzia maandalizi kuelekea mchezo husika.

Kwenye mkutano huo ambao ulifanyika leo Disemba 10, mwaka huu majira ya saa 6 mchana kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, uliopo Ilala, Dar es Salaam uliudhuliwa na kocha wa Yanga tu, Mohammed Nasreddine Nabi.

Kocha huyo wa klabu ya Simba alifika mchana akiambatana na maafisa wa klabu hiyo kitengo cha Habari na mawasiliano na mara baada ya Nabi kumaliza kuongea na waandishi wa Habari, maafisa hao waliingia kwenye ukumbi huo na kutanga bango hilo lenye nembo ya Gsm kutolewa, lakini jambo hilo halikufananikiwa na wakaamua kumuondoa kocha wao kwenye viunga hivyo.

Sintofahamu hii inatokea ikiwa siku chache toka klabu ya Simba ilipoandika barua kwenda Bodi ya Ligi ya kutaka ufafanuzi wa mkataba ambao Tff uliingia dhidi ya kampuni ya Gsm ya udhamini mwenza wa Ligi Kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!