Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari Ununuzi wa Meli: Bosi mpya bandari matatani
Habari

Ununuzi wa Meli: Bosi mpya bandari matatani

Spread the love

 

MKURUGENZI wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Erick Hamissi, anatajwa kuwa mmoja wa watuhumiwa muhimu kwenye mradi wa kitapeli wa ujenzi wa meli tano, zenye thamani Sh.438.83 bilioni, katika eneo la maziwa na bahari ya Hindi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinaeleza, wakati mchakato wa kumtafuta mzabuni unafanyika, Hamissi ndiye alikuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL).

Ufisadi katika mradi wa ujenzi wa meli nchini, ulitangazwa kwa mara ya kwanza hadharani na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani, Jumamosi iliyopita, akizindua upanuzi wa gati katika bandari ya Dar es Salaam.

Kampuni ya Serikali ya MSCL, ambayo wakati huo Hamissi alikuwa Mtendaji Mkuu, ndiyo iliyosimamia mchakato wa upatikanaji wa mzabuni wa ujenzi wa meli hizo, ambao Rais Samia alisema, “mkataba wake, hauna manufaa kwa nchi.”

Undani zaidi wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Ijumaa, tarehe 10 Desemba 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!