Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Watahiniwa 393 wafutiwa matokeo mtihani darasa la saba
Elimu

Watahiniwa 393 wafutiwa matokeo mtihani darasa la saba

Spread the love

 

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA), limefuta matokeo ya watahiniwa 393, waliobainika kufanya udanganyifu wakati wa kufanyika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 30 Oktoba 2021 na Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde, akitangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba, uliofanyika tarehe 8 na 9 Septemba mwaka huu.

“NECTA limeyafuta matokeo ya watahiniwa 393, waliobainika kufanya udanganyifu wakati wa kufanyika mitihani hii ya kumaliza elimu ya msingi, kwa mujibu wa kifungu cha 30 (2B ) cha kanuni za mitihani,” amesema Dk. Msonde.

Aidha, Dk. Msonde amesema NECTA limezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 128, ambao walishindwa kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kuugua au kupata matatizo. Hivyo, wamepewa fursa ya kurudia kufanya mtihani 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!