Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Watahiniwa 393 wafutiwa matokeo mtihani darasa la saba
Elimu

Watahiniwa 393 wafutiwa matokeo mtihani darasa la saba

Spread the love

 

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA), limefuta matokeo ya watahiniwa 393, waliobainika kufanya udanganyifu wakati wa kufanyika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 30 Oktoba 2021 na Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde, akitangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba, uliofanyika tarehe 8 na 9 Septemba mwaka huu.

“NECTA limeyafuta matokeo ya watahiniwa 393, waliobainika kufanya udanganyifu wakati wa kufanyika mitihani hii ya kumaliza elimu ya msingi, kwa mujibu wa kifungu cha 30 (2B ) cha kanuni za mitihani,” amesema Dk. Msonde.

Aidha, Dk. Msonde amesema NECTA limezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 128, ambao walishindwa kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kuugua au kupata matatizo. Hivyo, wamepewa fursa ya kurudia kufanya mtihani 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!