Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari Simba yamtimua Gomes, Hitimana arithi mikoba yake
HabariMichezoTangulizi

Simba yamtimua Gomes, Hitimana arithi mikoba yake

Didier Gomes da Rosa
Spread the love

 

KLABU ya Soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam, imevunja mkataba na aliyekuwa kocha wake Mkuu, Didier Gomes Da Rosa, mara baada ya makubaliano ya pande zote mbili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Maamuzi hayo yamefikiwa mara baada ya timu hiyo kuondolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana kwenye mchezo uliopigwa jumapili Oktoba 24, 2021 kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo imeeleza kuwa, uongozi wa klabu hiyo umeridhia ombi la Gomes juu ya kuachana na Simba kuanzia leo Oktoba 26, 2021.

Mara baada ya kujiweka pembeni nafasi ya Gomes kwenye timu hiyo, itashikiliwa na Thierry Hitimana kama kocha wa muda huku akisaidia na Seleman Matola, kama kocha wake msaidizi.

Aliyekuwa kocha wa makipa wa klabu ya Simba Milton Nienov

Aidha klabu hiyo pia imefanya marekebisho kwenye benchi lake la ufundi kwa kusitiosha mkataba wa aliyekuwa kocha wa makipa Milton Nienov pamoja na kocha wa viungo Aden Zrane.

Gomes alijiunga na Simba January, mwaka huu akitokea kwenye klabu ya El Merreikh ya nchini Sudan, ambapo alikuja kuchukua nafasi ya Sven Vandebroeck aliyetimkia nchini Morocco.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!