Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mzee Mangula ahimiza vikao kufanya maamuzi
Habari za Siasa

Mzee Mangula ahimiza vikao kufanya maamuzi

Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapiduzi (CCM), Mzee Phillip Mangula, amesema vikao ni muhimu katika kutafuta makubaliano na kujenga umoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mzee Mangula ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 12 Oktoba 2021, akitoa mada ya mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere katika kudumisha amani na umoja kwa maendeleo ya jamii, kwenye kongamano la kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha muasisi huyo wa Taifa la Tanzania, lililofanyika jijini Dar es Salaam.

“Vikao vinajenga umoja kuhusu hayo mnayotaka kufanyia uamuzi, tofauti ya mawazo ndiyo kujadiliana,  kutoa mawazo yako mkubaliane kisha linakuwa lenu mnajenga umoja,” amesema Mzee Mangula.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini Tanzania, amesema hata Mwalimu Nyerere alifanikiwa kujenga umoja kwa kufanya majadiliano  kwenye vikao.

” Mwalimu Nyerere alijenga umoja wa viongozi na usingeweza kupatikana huu umoja bila kukutana, alijenga mfumo msingi wa kukutana katika vikao ndani ya chama chake,  ana wazo lake analeta wanalikubali linakuwa wazo letu. Mmetofautiana katika mawazo kila mtu ameleta mawazo yake lakini mkiongozwa na viongozi wa kikao chenu mnafika muafaka mnakubaliana,” amesema Mzee Mangula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!