Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mzee Mangula ahimiza vikao kufanya maamuzi
Habari za Siasa

Mzee Mangula ahimiza vikao kufanya maamuzi

Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapiduzi (CCM), Mzee Phillip Mangula, amesema vikao ni muhimu katika kutafuta makubaliano na kujenga umoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mzee Mangula ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 12 Oktoba 2021, akitoa mada ya mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere katika kudumisha amani na umoja kwa maendeleo ya jamii, kwenye kongamano la kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha muasisi huyo wa Taifa la Tanzania, lililofanyika jijini Dar es Salaam.

“Vikao vinajenga umoja kuhusu hayo mnayotaka kufanyia uamuzi, tofauti ya mawazo ndiyo kujadiliana,  kutoa mawazo yako mkubaliane kisha linakuwa lenu mnajenga umoja,” amesema Mzee Mangula.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini Tanzania, amesema hata Mwalimu Nyerere alifanikiwa kujenga umoja kwa kufanya majadiliano  kwenye vikao.

” Mwalimu Nyerere alijenga umoja wa viongozi na usingeweza kupatikana huu umoja bila kukutana, alijenga mfumo msingi wa kukutana katika vikao ndani ya chama chake,  ana wazo lake analeta wanalikubali linakuwa wazo letu. Mmetofautiana katika mawazo kila mtu ameleta mawazo yake lakini mkiongozwa na viongozi wa kikao chenu mnafika muafaka mnakubaliana,” amesema Mzee Mangula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!