Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa aziagiza wizara, halmashauri ziimarishe mazingira uchumi shirikishi
Habari za Siasa

Majaliwa aziagiza wizara, halmashauri ziimarishe mazingira uchumi shirikishi

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, ameziagiza wizara, halmashauri na taasisi za Serikali na binafsi, ziimarishe mazingira ya uchumi shirikishi ili kukuza kipato cha wananchi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Waziri Majaliwa ametoa agizo hilo leo Jumatatu, tarehe 4 Oktoba 2021, katika kongamano la tano la kitaifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, lililofanyika jijini Dodoma.

“Naagiza wizara za kisekta na uchumi ziimarishe kiumdombinu muhimu kama ya kilimo, uvuvi, mifugo, biashara na uwekezaji, ili kukuza ajira na kipato cha mtu mmoja mmoja. Halamshauri zihakikishe hafua za uwezeshaji wananchi kiuchumi zinatenegwa bajeti na kuwajengea uwezo maafisa biashara,” amesema Waziri Majaliwa.

Aidha, Waziri Majaliwa ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango, izisimamie taasisi za fedha ili zitoe huduma za kifedha, ikiwemo mitaji kwa masharti nafuu hasa kwenye maeneo ya vijijini na pembezoni mwa nchi.

Waziri Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuimarisha mazingira ya ukuzaji uchumi jumuishi na kuvutia uwekezaji, kwa lengo la kupanua shughuli hizo.

Wakati huo huo, Waziri Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa nchini, kwa kushirikiana na wafanyabiashara ndogondogo, ikiwemo wamachinga, kutenga maeneo mazuri ya ufanyaji biashara zao, ambayo itakuwa rahisi wananchi kuyafikia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!