Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Mchezaji aliyeishiwa nguvu baada ya kufunga, arejea kambini
Michezo

Mchezaji aliyeishiwa nguvu baada ya kufunga, arejea kambini

Crispin Ngush
Spread the love

 

CRISPIN Ngush, mchezaji wa Mbeya Kwanza nchini Tanzania, aliyefunga bao maridadi kisha kuishiwa nguvu na kupelekwa hospitalini, ameruhusiwa kurejea kambini kuungana na wenzake. Anaripoti Damas Ndembela,TUDARCo … (endelea).

Ngush alifunga bao hilo dakika ya 87 dhidi ya Mbeya City jana Jumapili, tarehe 3 Oktoba 2021, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/22, Uwanja wa Sokoine jijini humo.

Lilikuwa ni bao la kushangaza la ‘bicycle-kick’ na kuinusuru timu yake kufungwa. Lilikuwa ni bao la kusawazisha na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa 2-2 na kuwafanya kugawana pointi.

Mara baada ya kufunga bao hilo, Ngush alikimbia akishangilia na kuruka sarakasi kisha alianguka china na kuchukuliwa na kupelekwa hospitalini.

Asubuhi leo Jumatatu, katika ukurasa wa kijamii wa Twitter wa Mbeya Kwanza iliyopanda daraja msimu huu, imeweka picha ya Ngush kuzungumzia hali ya mchezaji wake.

“Mpachika mabao wetu Crispin Ngush, aliyeishiwa nguvu baada ya kutufungua bao la kusawazisha na bao lake la pili jana na kukimbizwa Hospital, anaendelea vizuri na ameshajiunga na wenzake kambini lakini akiwa chini ya uangalizi wa Daktari. Tunashuru kwa sapoti yenu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!