Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watanzania laki 4 wachanjwa, milioni 2 zaagiwa China
AfyaHabari za SiasaTangulizi

Watanzania laki 4 wachanjwa, milioni 2 zaagiwa China

Spread the love

 

MSEMAJI Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema, idadi ya wananchi waliochanjwa chanjo ya corona imefikia 400,000. Anaripoti Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).

Msigwa amesema hayo leo Jumapili, tarehe 26 Septemba 2021, wakati akizungumza na waandishi wa habari, mkoani Singida kutoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa mambo mbalimbali yaliyofanywa na serikali.

Chanjo hiyo ni kati ya milioni moja aina ya Johnson & Johnson, msaada kutoka nchini Marekani ambayo, ilizinduliwa tarehe 28 Julai 2021 na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Dar es Salaam kwa yeye mwenyewe kuchanjwa.

Msigwa amesema, tangu zoezi za uchanjaji wa chanjo ya corona ilipoanza, wananchi 400,000 wamechanjwa kati ya chanjo milioni moja iliyowasili nchini “kwa kasi tunayokwenda nayo haziwezi kuchukua muda mrefu.”

Amesema, hawataki kuona Mtanzania aliyetayari kupata chanjo anapata shida ya kwenda sehemu ya kuchanjwana hivyo vituo vya chanjo vimeongezwa kutoka mia tano na kufikia zaidi ya elfu sita kwenye vituo vya mabasi, masoko, vituo vya kupima uzito magari na Mwenge wa uhuru.

“Juhudi za mapambano ya corona inaendelea na sasa kila kituo cha chanjo zaidi ya elfu sita nchini napo wanatoa chanjo ya corona kama vituo vya mabasi na hata jana kwenye mchezo wa watani,” amesema Msigwa

Msemaji huyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo amesema, “Serikali imeagiza chanjo nyingine ya corona milioni mbili kutoka China, hizi zitakuwa dozi mara mbili.”

Ametumia fursa hiyo, kuwaomba wananchi kujitokeza maeneo yenye chanjo na kuchanjwa kwani “sehemu kubwa wanaopumua kwa msaada wa mashine kwenye hospitali wengi ni ambao hawakuchanjwa.”

“Usipochanjwa yakikupata hoi na hata idadi ya vifo, vingi ni wale ambao hawakuchanja,” amesema Msigwa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

error: Content is protected !!