Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watanzania laki 4 wachanjwa, milioni 2 zaagiwa China
AfyaHabari za SiasaTangulizi

Watanzania laki 4 wachanjwa, milioni 2 zaagiwa China

Spread the love

 

MSEMAJI Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema, idadi ya wananchi waliochanjwa chanjo ya corona imefikia 400,000. Anaripoti Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).

Msigwa amesema hayo leo Jumapili, tarehe 26 Septemba 2021, wakati akizungumza na waandishi wa habari, mkoani Singida kutoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa mambo mbalimbali yaliyofanywa na serikali.

Chanjo hiyo ni kati ya milioni moja aina ya Johnson & Johnson, msaada kutoka nchini Marekani ambayo, ilizinduliwa tarehe 28 Julai 2021 na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Dar es Salaam kwa yeye mwenyewe kuchanjwa.

Msigwa amesema, tangu zoezi za uchanjaji wa chanjo ya corona ilipoanza, wananchi 400,000 wamechanjwa kati ya chanjo milioni moja iliyowasili nchini “kwa kasi tunayokwenda nayo haziwezi kuchukua muda mrefu.”

Amesema, hawataki kuona Mtanzania aliyetayari kupata chanjo anapata shida ya kwenda sehemu ya kuchanjwana hivyo vituo vya chanjo vimeongezwa kutoka mia tano na kufikia zaidi ya elfu sita kwenye vituo vya mabasi, masoko, vituo vya kupima uzito magari na Mwenge wa uhuru.

“Juhudi za mapambano ya corona inaendelea na sasa kila kituo cha chanjo zaidi ya elfu sita nchini napo wanatoa chanjo ya corona kama vituo vya mabasi na hata jana kwenye mchezo wa watani,” amesema Msigwa

Msemaji huyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo amesema, “Serikali imeagiza chanjo nyingine ya corona milioni mbili kutoka China, hizi zitakuwa dozi mara mbili.”

Ametumia fursa hiyo, kuwaomba wananchi kujitokeza maeneo yenye chanjo na kuchanjwa kwani “sehemu kubwa wanaopumua kwa msaada wa mashine kwenye hospitali wengi ni ambao hawakuchanjwa.”

“Usipochanjwa yakikupata hoi na hata idadi ya vifo, vingi ni wale ambao hawakuchanja,” amesema Msigwa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!