Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua viongozi akiwa Marekani
Habari za Siasa

Rais Samia ateua viongozi akiwa Marekani

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wawili. Anaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo … (endelea).

Taarifa ya uteuzi imefanyika leo Jumatatu, tarehe 20 Septemba 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Rais Samia amefanya uteuzi huo akiwa ziarani nchini Marekani alikokwenda kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Walioteuliwa ni, Yona Killagane kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO).

Pia, amemteua Mathew Modest Kirama kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma (PSC).

Kabla ya uteuzi huu Kirama alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma (DE), Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Kirama anachukua nafasi ya Nyakimura Mathias Muhoji ambaye amestaafu.

Uteuzi huo umeanza tarehe 18 Septemba, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!