DAKTARI mmoja mkazi wa Nakuru nchini Kenya anadaiwa kuwaua wanawe wawili kisha kujaribu kujitoa uhai usiku wa Jumamosi tarehe 18 Septemba mwaka huu. Anaripoti Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).
Daktari huyo aliyefahamika kwa jina la James Gakara ambaye ni daktari wa uzazi katika hospitali ya Optimum Current Nakuru anadaiwa kuwadunga watoto wake wenye umri wa miaka 5 na 3 sindano yenye sumu na kufariki papo hapo.
Askari upelelezi walioitwa na majirani kuchunguza sababu za daktari huyo kujifungia ndani na watoto wake, jambo lisilo la kawaida, walikuta miili ya watoto hao ikiwa imelala kitandani huku povu likiwatoka midomoni.
Mshukiwa pia alikutwa akiwa amelala kitandani mwake akiwa na povu mdomoni ila hakuwa amekata roho.
Alikimbizwa katika hospitali ya Nakuru ambapo madaktari walinusuru maisha yake.
Dawa za zilizokutwa kwenye sirinji zilizokuwa zimetumika na kisu chenye makali ni baadhi ya vitu ambavyo vilipatikana kwenye eneo la tukio.
Kwa sasa mshukiwa anaendelea kupata nafuu hospitalini huku akisubiri kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo la kikatili.
Leave a comment