Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kutambulisha Benchi jipya la ufundi
Michezo

Yanga kutambulisha Benchi jipya la ufundi

Spread the love

 

KLABU ya Soka ya Yanga itaweka wazi benchi lake la ufundi kwenye kilele cha siku ya Mwananchi, mara baada ya kuwepo kwa taarifa za kuvunja mkataba kwa kocha wao msaidizi Sighr Hamad na mtaalamu wa mazoezi ya viungo Jawad Sabri. Anaripoti Wiston Josia na Ndelem Damas/TUDARCo…(endelea)

Timu hiyo kwa sasa imeweka kambi Rabat, nchini Morocco kwa ajili ya kufanya maandalizi ya msimu (Pre-Season), chini ya kocha wao Mkuu, Mohammed Nasreddin Nabi.

Yanga ambao watarejea nchini Agosti 27, kujiandaa na Tamasha lao kubwa la siku ya Mwananchi ambalo litafanyika Agosti 28, Mwaka huu, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Hassan Bumbuli, Afisa Habari wa Yanga

Akizungumza na juu ya watu hao wa benchi la ufundi kuvunja mkataba, Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli alisema kuwa kuna baadhi yao wameshamaliza mikataba, hivyo wanaangalia

uwezekano wa kuwaongeza au kuachana nao, na siku ya kilele cha Tamasha hilo ndipo watakapojulikana rasmi.

“Mimi pia ni sehemu ya utambulisho siku hiyo, na utambulisho utakuwa mpaka kwenye benchi la ufundim kwa hiyo waandishi muwe wavumilivu”

“Kuna watu wamemaliza mkataba, kwa hiyo wanaweza kuwepo au wasiwepo, nap engine wanaweza kupewa mkataba mpya kama tukikubaliana kama tukikubaliana, tusipokubaliana hawata kuwepo” alisema Bumbuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!