Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Taliban waanza msako wa mahasimu wake
Kimataifa

Taliban waanza msako wa mahasimu wake

Spread the love

 

SIKU chache baada ya wanamgambo wa Taliban kuipindu Serikali ya Afghanistan, wanajeshi hao wameanza kusaka mahasimu wao. Anaripoti Noela Shila, TUDARCo, kwa msaada wa mitandao ya kimataifa … (endelea).

Taliban waliipindua Serikali hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Rais Ashraf Ghani, Jumapili ya tarehe 15 Agosti 2021, baada ya kuiteka Ikulu ya Afghanstan pamoja na miji muhimu 23 kati ya 34 nchini humo.

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC, wanamgambo hao baada ya kufanya mapinduzi hayo, wameanza kufanya msako wa nyumba kwa nyumba, kuwatafuta wapinzani wao ikiwemo watu waliofanya kazi na Jumuiya ya Kujihami (NATO) na Serikali ya Afghanistan, katika kuwaondoa madarakani mwaka 2001.

Taarifa ya msako huo imetolewa na Umoja wa Mataifa (UN), ukisema kwamba, Taliban wameanza kuingia nyumba kwa nyumba, kuwatafuta wapinzani wao, huku wakizitishia familia zao.

Christian Nellemann, aliyeandaa ripoti ya UN kuhusu matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu, unaofanywa na Taliban, amesema maisha ya watu wanaolengwa na wanamgambo hao, yako hatarini.

Kundi la wanamgambo hao wenye itikadi kali ya kiislamu, liliiongoza Afghanistan kuanzia 1996 hadi 2001, ambapo liling’olewa na majeshi ya mataifa ya kigeni ikiwamo Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

error: Content is protected !!