Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yavuta mwengine
MichezoTangulizi

Yanga yavuta mwengine

Spread the love

 

KLABU ya soka ya Yanga, imefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji Yusuph Athuman Akitokea klabu ya Biashara United, Mara iliyokuwa inashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mshambuliaji huyo ameingia mkataba wa miaka mitatu, kukipiga ndani ya Yanga ambapo alikuwepo hapo awali kwenye timu ya vijana.

Kwenye msimu wa 2020/21. Akiwa na kikosi cha Biashara United Yusuph alicheza jumla ya dakika 216, na kufanikiwa kufunga mabao 2, na kutoa pasi za mabao (assist) mbili.

Huu utakuwa usajili wa pili wa Yanga, ndani ya siku mbili mara baada ya kumtambulisha mshambuliaji kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Fiston Kalala Mayele.

Klabu hiyo inaendelea kuimarisha kikosi chake katika kuelekea msimu ujao wa mashindano, hasa Ligi Kuu Tanzania Bara, na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Walimu 5000 Songwe waililia CWT kuwanyima sare

Spread the loveZaidi ya walimu 5000 ambao ni wanachama wa Chama cha...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!