Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yavuta mwengine
MichezoTangulizi

Yanga yavuta mwengine

Spread the love

 

KLABU ya soka ya Yanga, imefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji Yusuph Athuman Akitokea klabu ya Biashara United, Mara iliyokuwa inashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mshambuliaji huyo ameingia mkataba wa miaka mitatu, kukipiga ndani ya Yanga ambapo alikuwepo hapo awali kwenye timu ya vijana.

Kwenye msimu wa 2020/21. Akiwa na kikosi cha Biashara United Yusuph alicheza jumla ya dakika 216, na kufanikiwa kufunga mabao 2, na kutoa pasi za mabao (assist) mbili.

Huu utakuwa usajili wa pili wa Yanga, ndani ya siku mbili mara baada ya kumtambulisha mshambuliaji kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Fiston Kalala Mayele.

Klabu hiyo inaendelea kuimarisha kikosi chake katika kuelekea msimu ujao wa mashindano, hasa Ligi Kuu Tanzania Bara, na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!