Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro azungumzia tuhuma za Mbowe, atoa onyo
Habari za SiasaTangulizi

IGP Sirro azungumzia tuhuma za Mbowe, atoa onyo

Spread the love

 

INSPEKTA Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amekitaka chama kikuu cha upinzani nchini humo, Chadema na wadau wengine, kuiachia mahakamana kesi inayomkabili mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mbowe na wenzake watatu, wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo la kupanga njama za ugaidi na uhujumu uchumi, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Tangu kukamatwa jijini Mwanza na kusafirishwa hadi Dar es Salaam na kisha kufikishwa mahakamani, wadau mbalimbali wa kutetea haki za binadamu wa ndani na nje ya Tanzania, wamekuwa wakipinga suala hilo.

Wameitaka dola kumwachia Mbowe aliyekamatwa usiku wa manane, akiwa hotelini kabla ya kushiriki kongamano la Katiba mpya ambalo hata hivyo halikufanyika.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema

Leo Jumatatu, tarehe 2 Agosti 2021, IGP Sirro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema, Mbowe na wenzake wamefikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Sirro amewaonya wale wote wanaokusudia kufanya maandamano tarehe 5 Agosti 2021, siku ambayo kesi hiyo itatajwa tena kutokufanya hivyo kwani “kuvamia mahakama ni sawa na kuvamia kambi ya jeshi, utakung’utwa tu, hivyo tuiachie mahakama ifanye kazi yake.”

“Chadema wanasema mwenyekiti wao (Mbowe) ameonewa, wanavyoona wao hawezi kufanya hivyo, sasa kama Mbowe ni mkweli na amamuamini Mungu waende wakamuulize jambo hili unasemaje.”

“Lakini kabla ya uchaguzi nilisema kuna watu wamepanga kuhakikisha uchaguzi haufanyiki, nilisema kuna watu wamepanga kulipua visima vya mafuta na nilisema wamepanga kuua viongozi na nilisema tutawakamata,” amesema Sirro

“Habari ya yeye wajue ni binadamu, anaweza kufanya makossa. Walitafuta vijana wetu tuliowafukuza jeshini, tumempeleka mahakamani tuwache mahakama itimize wajibu wake, habari za chama cha siasa, habari za viongozi wa dini, asasi za kiraia waache,” amesema Sirro

Katika kusisitiza hilo, Sirro amesema, “kama kweli ni mkweli mwenyekiti wao, na amaanimi Mungu waende wakamuulize, lakini wengine wanaosema sema ni sawa na jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, usiingie katika mtego, tusubiri mahakama ifanye kazi yake.”

Sirro amewaonya wanaotaka kuhatarisha usalama wa nchi kwamba serikali haitawaacha salama na “tuwaache wale watu wachache wanaotaka kupambana na serikali, lakini kama wameandaa kwenda Canada, Marekani waende ila hatutaruhusu kikundi cha watu.”

“Wale ambao wameambiwa wakusanyike kuja mahakamani, waelewe mahakaman ni eneo nyeti, Mahakama ni sawa na kituo cha polisi, ukitaka kuvamia utakung’utwa, Mbowe yuko mahakamani waiache ifanye kazi zake,” amesema

1 Comment

  • Huyu mgambo Sirro mjinga sana anajiona yeye ndio yupo juu ya sheria ktk utawala wa magufuli raia kibao walishikiliwa na jeshi hili hili la polisi na kubambikiwa kesi za uongo huku huyo mjinga mjinga mgambo Sirro akifumbia macho wajibu wake wa kulinda raia na mali zao ila yeye na utawala wa awamu ya tano walihusika kwa kkuuwa,kutesa,na kupora raia,malizao sasa wewe mjinga mjinga zirro unataka kutwambia nini fala wewe?..kama mbwai naiwe bwahi hii dunia sio yako wala ya babayako mamammayoooo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!