Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Majaliwa atoa maagizo wanufaika mafunzo ya ufundi
Elimu

Majaliwa atoa maagizo wanufaika mafunzo ya ufundi

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka vijana waliopata ufadhili wa Serikali kupitia programu maalum ya kupata mafunzo ya ufundi stadi watumie vizuri fursa hiyo ili wanufaike. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fungu la fedha kwa ajili ya kuwasomesha vijana katika fani mbalimbali za ufundi stadi kwa muda wa miezi sita.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana Jumapili, tarehe 1 Agosti 2021, wakati wa uzinduzi wa chuo cha Ufundi Stadi kilichopo katika kijiji cha Kipapa kata ya Lufilyo wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya.

“Kilichotuleta hapa ni kuja kushuhudia vijana wetu wa Kitanzania ambao wameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa lengo la kuwapatia ujuzi ili wakaendeleze kazi hizo.”

Alisema Tanzania nzima kuna vijana takribani 45,000 ambao wamesambazwa katika vyuo vyote vya Serikali na vya binafsi ambapo watapatiwa mafunzo ya ufundi stadi kwa miezi sita.

Majaliwa alisema, mbali na kupatiwa ujunzi katika vyuo hivyo pia vijana wengine wamepelekwa kwenye maeneo ya kutolea huduma kama za utalii, hoteli ili wapate ujuzi.

Alisema chuo hicho cha VETA Busokelo ni kimojawapo kati ya vyuo walivyovichagua ili kipokee vijana wa maeneo ya wilaya za Rungwe, Kyela, Chunya na Mbeya ili kuwapa ujuzi.

“Matarajio yangu vijana wote waliopata nafasi hii hawataipoteza, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anatamani kuona kila Mtanzania akijishughulisha na shughuli za ujasiriamali.”

Alisema mkakati wa Serikali kwa mwaka 2021 ni kusomesha vijana 80,000 ambapo asilimia 60 ya mafunzo hayo watayapata kwa vitendo na asilimia 40 watafundishwa darasani.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Pancras Bujulu alisema chuo cha Ufundi Stadi cha Busokelo kimedahili wanafunzi 127 ambao watapa mafunzo ya ufundi kupitia program hiyo.

Alisema kati ya wanafunzi hao 26 wanasomea ufundi seremala, 45 ushonaji nguo, 28 umeme wa majumbani, 18 ukarabati wa vitarakimishi na 10 utengenezaji wa vifaa vya kielektroniki.

Alisema mafanikio ya programu hiyo ni pamoja na kuwawezesha wanafunzi waliopata ujuzi kuweza kujiajiri katika fani za useremala, ushonaji, udereva na matumizi ya vitarakinishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!