Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Joto kali lauwa watu 130 Canada
Habari Mchanganyiko

Joto kali lauwa watu 130 Canada

Spread the love

 

WATU zaidi ya 130 wameripotiwa kufariki dunia nchini Canada, baada ya kuathiriwa na joto kali lililoikumba nchi hiyo tangu Jumatatu ya tarehe 28 Juni 2021. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mitandao hiyo, watu hao walifariki dunia kati ya Jumatatu hadi leo Jumatano tarehe 30 Juni 2021, ambapo wazee wanaongoza katika idadi ya vifo hivyo.

Jeshi la Polisi nchini Canada, limesema idadi kubwa ya vifo ilitokea katika Mji wa Vancouver uliopo Wilaya ya Burnaby, ambapo watu 69 wamefariki dunia.

Mamlaka nchini Canada zinasema, kiwango hicho cha juu cha joto hakijawahi kushuhudiwa nchini humo, ambapo katika siku tatu mfululizo kiwango hicho kilikuwa nyuzi joto 49.9.

Maeneo yanayotajwa kuathirika na joto hilo ni Lytton, British Columbia, Alberta, Saskatchewan na Yukon.

Inadaiwa kuwa, Canada iliwahi kukabiliwa na changamoto hiyo miaka kadhaa iliyopita, lakini kiwango cha juu cha joto kilikuwa nyuzi 45.

Kufuatia changamoto hiyo, wananchi nchini Canada wametakiwa kuchukua tahadhari za kujikinga na athari za joto kali, huku wazee wakipewa kipaumbele katika uangalizi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!