Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia Mhandisi Mfugale
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia amlilia Mhandisi Mfugale

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Patrick Mfugale. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mhandisi Mfugale, alifikwa na mauti jana Jumanne, saa 5:00 asubuhi, tarehe 29 Juni 2021, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.

Hadi anafikwa na mauti, amehudumu nafasi ya mtendaji mkuu kwa zaidi ya miaka kumi, kuanzia tarehe 23 Mei 2011, akiwa amesimamia ujenzi wa barabara zaidi ya kilomita 1,400 na madaraka mbalimbali yakiwemo ya juu.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia ameandika “Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Mhandisi Patrick Mfugale (Mtendaji Mkuu-TANROADS).”

“Nitaukumbuka mchango mkubwa katika ujenzi wa miundombinu yetu hasa barabara, madaraja, reli na umeme.”

“Pole kwa Familia na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina.”

Awali, jana Jumanne usiku, taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ilisema, taratibu za mazishi zitatangazwa baadae.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!