Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Joto kali lauwa watu 130 Canada
Habari Mchanganyiko

Joto kali lauwa watu 130 Canada

Spread the love

 

WATU zaidi ya 130 wameripotiwa kufariki dunia nchini Canada, baada ya kuathiriwa na joto kali lililoikumba nchi hiyo tangu Jumatatu ya tarehe 28 Juni 2021. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mitandao hiyo, watu hao walifariki dunia kati ya Jumatatu hadi leo Jumatano tarehe 30 Juni 2021, ambapo wazee wanaongoza katika idadi ya vifo hivyo.

Jeshi la Polisi nchini Canada, limesema idadi kubwa ya vifo ilitokea katika Mji wa Vancouver uliopo Wilaya ya Burnaby, ambapo watu 69 wamefariki dunia.

Mamlaka nchini Canada zinasema, kiwango hicho cha juu cha joto hakijawahi kushuhudiwa nchini humo, ambapo katika siku tatu mfululizo kiwango hicho kilikuwa nyuzi joto 49.9.

Maeneo yanayotajwa kuathirika na joto hilo ni Lytton, British Columbia, Alberta, Saskatchewan na Yukon.

Inadaiwa kuwa, Canada iliwahi kukabiliwa na changamoto hiyo miaka kadhaa iliyopita, lakini kiwango cha juu cha joto kilikuwa nyuzi 45.

Kufuatia changamoto hiyo, wananchi nchini Canada wametakiwa kuchukua tahadhari za kujikinga na athari za joto kali, huku wazee wakipewa kipaumbele katika uangalizi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!