Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mama Salma Kikwete alilia maji jimboni mwake, waziri amjibu
Habari Mchanganyiko

Mama Salma Kikwete alilia maji jimboni mwake, waziri amjibu

Mama Salma Kikwete
Spread the love

 

MBUNGE wa Mchinga mkoani Lindi (CCM), Mama Salma Kikwete,ameiomba Serikali ipeleke maji safi na salama kwa wananchi wa jimbo hilo. Anaripoti Mwandishi Wetyu, Dodoma…(endelea).

Mama Salma ametoa ombi hilo leo Jumanne, tarehe 29 Juni 2021, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

Mke huyo wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, ameiomba Serikali ilifikirie jimbo lake, kwa kuwa linakabiliwa na uhaba wa maji safi na salama, huku akiishauri itoe maji katika chanzo cha Ng’apa, kisha iyasambaze jimboni humo.

“Maji ni uhai kwa viumbe vyote, ni muhimu kwa ustawi. Naomba kuuliza swali langu, jimbo langu la Mchinga halina maji safi na salama. Sasa ningeomba jimbo hili lifikiriwe kwa umakini mkubwa, kupata maji safi na salama kutoka chanzo kikubwa cha Ng’apa,” amesema Mama Salma na kuongeza:

“Je, ni lini maji safi na salama yatapelekwa Mchinga, kwa wananchi wa jimbo hio?”

Akijibu swali hilo, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema atafika katika jimbo hilo, ili aangalie namna ya kutatua changamoto zake za huduma ya maji.

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso

“Najua changamoto za watu wake, siku zote anayelala na mgonjwa anajua mhemo wa ugonjwa. Naomba nimpe upendeleo maalumu, moja kufika kwanza katika jimbo lake,” amesema Aweso na kuongeza:

“Pili tunatambua tuna chanzo toshelevu cha Ng’apa, tumejenga mradi wa maji Lindi. Tunataka tuyatoe maji ya Ng’apa ili tuhakikishe yanafika Mchinga ili wananchi waondokane na matatizo ya maji.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kamati Kuu Chadema kuketi Mei 11

Spread the loveKAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari Mchanganyiko

Mradi uliotaka kumng’oa madarakani Dk. Mpango waanza majaribio

Spread the loveMRADI wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe, ambao Makamu wa Rais, Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

error: Content is protected !!