Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Adhabu ya mkwepa kodi yaanikwa
Habari za Siasa

Adhabu ya mkwepa kodi yaanikwa

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

MFANYABIASHARA ama mtoa huduma ambaye atabainika kuwepa kulipa kodi, akikamatwa atalazimika kulipa asilimia 100 ya kodi aliyotakiwa kulipa kama adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwamba, kodi hiyo itakuwa mara mbili ya kodi anayodaiwa mteja, ambapo mapendekezo ya kuwekwa kwa adhabu hiyo yamefanywa na wabunge wa Bunge la Jamhuri.

Dk Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango akijibu hoja wakati wa kuhitimisha majadiliano ya Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2021, amesema baada ya kusikia hoja za wabunge, serikali imeamua kuchukua ushauri kwa kuweka kifungu kipya cha kubana ukwepaji kodi.

Dk. Mwigulu amesema, makubaliano yaliyofikiwa katika kikao kati ya serikali na kamati ya bunge, ni kufanya mabadiliko kwenye tuliokuwa tumependekeza kuweka asilimia 75, wamependekeza kuwa asilimia 100 ya kodi iliyotakiwa kutozwa.

“Kwa maana hiyo, kodi itakuwa imezidishwa mara mbili ya iliyotakiwa kutozwa kama mtu huyo atakuwa amekwepa, kwa hiyo sisi kama serikali tunapokea maoni ya wa waheshimiwa wabunge na kamati ambayo ni mwakilishi wa Bunge,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!