Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona-19: WHO, Tanzania kukaameza moja
Afya

Corona-19: WHO, Tanzania kukaameza moja

Dk. Dorothy Gwajima, Waziri wa Afya wa Tanzania
Spread the love

 

TANZANIA na Shirika la Afya Duniani (WHO), wanatarajia kukaa meza moja ili kuangalia namna ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Vikao hivyo vya kitaaluma vimepangwa kuanza Julai 2021, ambapo tayari serikali imezindua Mpango Mkakati wa Miaka mitano wa Sekta ya Afya (2021-2025) unaotarajiwa kugharimu Sh. 47 trilioni.

Mpango huo ulizinduliwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima, jijini Dar es Salaam.

Alisema, katika kukabiliana na wimbi la tatu la mlipuko wa ugonjwa huo, Julai 2021 serikali itahusisha vikao vya kitaalamu chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Serikali na Uenyekiti mwenza wa Mwakilishi Mkazi wa WHO.

“Sambamba na kuanza vikao hivyo ninaelekeza vikao vya kila mhimili katika Mpango wa Taifa wa Udhibiti Ugonjwa wa UVIKO-19 vianze kwa lengo la kudhibiti ugonjwa huo nchini,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!