Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Mbunge alia ukosefu X-Ray, Serikali yatoa agizo
Afya

Mbunge alia ukosefu X-Ray, Serikali yatoa agizo

Spread the love

 

WIZARA ya Ofisi ya Rais-Tamisemi, imeiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, itumie mapato yake ya ndani, kununua kipimo cha kuchunguza mwili kwa kutumia mawimbi ya sauti (Ultrasound). Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo Jumatatu tarehe 24 Mei 2021, na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, Dk. Festo Dugange, akimjibu Mbunge Viti Maalum (CCM) mkoani Kigoma, Josephine Genzabuke.

Katika swali lake, Genzabuke alihoji lini Serikali itakipatia kituo cha Afya cha Muyama, kilichomo wilayani Buhigwe, vifaa vya Ultrasound na X-Ray.

Akijibu swali hilo, Dk. Dugange amesema kama halmashauri hiyo haina mapato ya kutosha kununua kifaa hicho cha uchunguzi , ikope katika Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

“Kituo cha Afya cha Muyana hakitoi huduma ya uchunguzi wa X-Ray na Ultrasound, kutokana na ukosefu wa majengo na vifaa hivyo. Serikali inamuelekeza mganga kununua Ultrasound kupitia mapato ya ndani,” amesema Dk. Dugange.

Kuhusu X-Ray, Dk. Dugange amesema Serikali inajipanga kununua kipimo hicho.

“Ultrasound inunuliwe wakati Serikali Kuu ikitafuta fedha kwa ajili ya kununu X-Ray. Aidha, ikiwa mapato ya ndani ya halmashuri hayatoshelezi, Serikali inamshauri mkurugenzi kukopa fedha kupitia NHIF na kununua mashine ya Ultrasound,” amesema Dk. Dugange.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

error: Content is protected !!