Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Membe amshika pabaya Cyprian Musiba
Habari Mchanganyiko

Membe amshika pabaya Cyprian Musiba

Cyprian Musiba
Spread the love

 

WAZIRI wa zamani wa Mambo ya Nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, wa Tanzania, Bernard Kamilius Membe, yuko mbioni kushinda shauri lake alilofungua mahakamani dhidi ya Cyprian Musiba na gazeti lake la Tanzanite. Anaripoti Yusuph Katimba, Dar es Salaam … (endelea).

Membe amefungua shauri hilo la madai dhidi ya Musiba, katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam. Anamtuhumu Musiba, kumchafua na kumvunjia hadhi yake.

Kwa mujibu wa rekodi zilizopo mahakamani, kesi hiyo, itaanza kusikilizwa upande mmoja, kuanzia tarehe 24 Juni 2021, mbele ya Jaji Joaquine De- Mello.

Bernard Membe

Jaji De-Mello, ametoa uamuzi huo baada ya mawakili wa Membe, kutaka utekelezaji wa uamuzi wa mahakama, kusikiliza kesi hiyo upande mmoja.

Mahakama Kuu, imempa siku saba mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba na wachapishaji wa gazeti hilo wawe wamewasilisha majibu dhidi ya madai ya Membe anayetaka kulipwa Sh. 10 bilioni.

Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema la leo Jumamosi, tarehe 22 Mei 2021

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!