Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Membe amshika pabaya Cyprian Musiba
Habari Mchanganyiko

Membe amshika pabaya Cyprian Musiba

Cyprian Musiba
Spread the love

 

WAZIRI wa zamani wa Mambo ya Nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, wa Tanzania, Bernard Kamilius Membe, yuko mbioni kushinda shauri lake alilofungua mahakamani dhidi ya Cyprian Musiba na gazeti lake la Tanzanite. Anaripoti Yusuph Katimba, Dar es Salaam … (endelea).

Membe amefungua shauri hilo la madai dhidi ya Musiba, katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam. Anamtuhumu Musiba, kumchafua na kumvunjia hadhi yake.

Kwa mujibu wa rekodi zilizopo mahakamani, kesi hiyo, itaanza kusikilizwa upande mmoja, kuanzia tarehe 24 Juni 2021, mbele ya Jaji Joaquine De- Mello.

Bernard Membe

Jaji De-Mello, ametoa uamuzi huo baada ya mawakili wa Membe, kutaka utekelezaji wa uamuzi wa mahakama, kusikiliza kesi hiyo upande mmoja.

Mahakama Kuu, imempa siku saba mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba na wachapishaji wa gazeti hilo wawe wamewasilisha majibu dhidi ya madai ya Membe anayetaka kulipwa Sh. 10 bilioni.

Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema la leo Jumamosi, tarehe 22 Mei 2021

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!