Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga na Mwadui, Simba na Dodoma Jiji, robo fainali Kombe la Shirikisho
MichezoTangulizi

Yanga na Mwadui, Simba na Dodoma Jiji, robo fainali Kombe la Shirikisho

Spread the love

RATIBA ya michuano ya Kombe la Azam Federation CUP (ASFC) nchini Tanzania, hatua ya robo fainali, itashuhudia Yanga ikisafiri kwenda Shinyanga kuwavaa Mwadui FC. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wakati Yanga ikisafiri, watani zao Simba, mabingwa watetezi wa michuano hiyo, itakuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, kuwaalika Dodoma Jiji.

Ratiba hiyo, imepangwa leo Jumanne, tarehe 11 Mei 2021, huku timu zingine kwenye hatua hiyo ya robo fainali ni Biashara United itatumia uwanja wake wa Karume, Mkoa wa Mara kuwaalika Namungo FC ya mkoani Lindi.

Rhino Rangers yenyewe itavaana na Azam FC. Michezo hiyo ya robo fainali, itachezwa kati ya tarehe 25 hadi 27 Mei 2021.

Mshindi kati ya Simba dhidi ya Dodoma Jiji, atavaana na mshindi kati ya Rhino Rangers dhidi ya Azam FC huku Biashara United dhidi ya Namungo watacheza na mshindi kati ya Mwadui FC dhidi ya Yanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

error: Content is protected !!