Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watumishi 99 wadai milioni 300, Silinde atoa maagizo
Habari za Siasa

Watumishi 99 wadai milioni 300, Silinde atoa maagizo

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

NASHON Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini (CCM), amehoji lini watumishi waliohamishiwa halmashauri ya Uvinza kutoka Kigoma Vijijini watalipwa stahiki zao. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Bidyanguze amehoji hayo leo Ijumaa, tarehe 30 April 2021, bungeni jijini Dodoma, katika swali lake akisema, “je ni lini watumishi waliohamishiwa Halmashauri ya Uvinza kutoka Halmashauri ya Kigoma Vijijini watalipwa stahiki zao?”

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, David Silinde amesema, halmashauri ya Wilaya Uvinza ina watumishi 99, wanaostahili kulipwa stahiki za uhamisho kufuatia kuhamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza.

“Katika mwaka wa fedha 2013/14, kiasi cha Sh.319.89 milioni kinahitajika ili kullipa madeni hayo ya watumishi,” ameeleza Tamisemi.

“Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, ilipaswa kutenga fedha katika mapato yake ya ndani ili kulipa madeni hayo jambo ambalo halijafanywa takriban miaka minane.”

“Namuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, kutenga fedha katika mapato ya ndani ya Halmashauri na kulipa madeni hayo,” amesema Silinde

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!