Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watumishi 99 wadai milioni 300, Silinde atoa maagizo
Habari za Siasa

Watumishi 99 wadai milioni 300, Silinde atoa maagizo

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

NASHON Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini (CCM), amehoji lini watumishi waliohamishiwa halmashauri ya Uvinza kutoka Kigoma Vijijini watalipwa stahiki zao. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Bidyanguze amehoji hayo leo Ijumaa, tarehe 30 April 2021, bungeni jijini Dodoma, katika swali lake akisema, “je ni lini watumishi waliohamishiwa Halmashauri ya Uvinza kutoka Halmashauri ya Kigoma Vijijini watalipwa stahiki zao?”

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, David Silinde amesema, halmashauri ya Wilaya Uvinza ina watumishi 99, wanaostahili kulipwa stahiki za uhamisho kufuatia kuhamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza.

“Katika mwaka wa fedha 2013/14, kiasi cha Sh.319.89 milioni kinahitajika ili kullipa madeni hayo ya watumishi,” ameeleza Tamisemi.

“Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, ilipaswa kutenga fedha katika mapato yake ya ndani ili kulipa madeni hayo jambo ambalo halijafanywa takriban miaka minane.”

“Namuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, kutenga fedha katika mapato ya ndani ya Halmashauri na kulipa madeni hayo,” amesema Silinde

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!