Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo ‘Europian Super League’ yaota mbawa baada ya timu sita kujitoa
Michezo

‘Europian Super League’ yaota mbawa baada ya timu sita kujitoa

Spread the love

 

MICHUANO ya Europian Super League haitafanyika tena baada ya klabu sita kutoka nchini England kujitoa kushiriki kutokana na mashabiki na wadau wa soka kupinga michuano hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Michuano hiyo ambayo ilikuwa imeanzishwa na timu 12 Barani Ulaya zikiwemo klabu sita kutoka England ambazo ni  Manchester United, Arsenal, Chelsea, Manchester City, Tottenham na Liverpool.

Mwenyekiti wa michuano hiyo, Andrea Agnelli amesema kuwa kujiondoa kwa timu hizo sita nchini England kwenye michuano hiyo kumefanya kushindwa kuendelea kama ilivyopangwa kutokana na shinikizo kubwa waliopata kutoka kwa mashabiki zao.

“Najaribu kubaki kushawishika na ubora wa huu mradi, Lakini nakubali na maanisha, sifikiri kama huu mradi (Europe Super League) utaendelea,” alisema kiongozi huyo.

Baada ya kutangazwa kutaka kuanzishwa kwa michuano hiyo mipya barani Ulaya ambayo ilipangwa kuchezwa katikati ya wiki mashabiki na wadau wengi wameonekana kutokubaliana na jambo hilo na kusema kuwa michuano hiyo haina afya kwa soka bali wamiliki wa klabu hizo wanaangalia fedha kulino mapenzi na mchezo husika.

Kabla ya michuano hiyo kuanza tayari benki JP Morgan kutoka America ilikuwa tayari kutoa kiasi cha dola za kimarekani bilioni 5, sawa na fedha za kitanzania trillion 11.5, huku dhumuni la kuanzisha michuano hiyo ni kuziondoa klabu kwenye ukata wa kifedha mara baada ya janga la Corona.

Ukiachilia timu hizo kutoka England klabu zingine zilizokuwa kwenye mipango na michuano hiyo ni Inter Milani, AC Millan, Juventus, Real Madrid, Barcelona na Atleticol Madrid.

Michuano hiyo ilipanga kushirikisha jumla ya timu 20, huku wadau wengi wa soka waliona kuwa ni kama njama za kutaka kuififisha michuano mikongwe ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!