Sunday , 26 March 2023
Home Kitengo Michezo ‘Europian Super League’ yaota mbawa baada ya timu sita kujitoa
Michezo

‘Europian Super League’ yaota mbawa baada ya timu sita kujitoa

Spread the love

 

MICHUANO ya Europian Super League haitafanyika tena baada ya klabu sita kutoka nchini England kujitoa kushiriki kutokana na mashabiki na wadau wa soka kupinga michuano hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Michuano hiyo ambayo ilikuwa imeanzishwa na timu 12 Barani Ulaya zikiwemo klabu sita kutoka England ambazo ni  Manchester United, Arsenal, Chelsea, Manchester City, Tottenham na Liverpool.

Mwenyekiti wa michuano hiyo, Andrea Agnelli amesema kuwa kujiondoa kwa timu hizo sita nchini England kwenye michuano hiyo kumefanya kushindwa kuendelea kama ilivyopangwa kutokana na shinikizo kubwa waliopata kutoka kwa mashabiki zao.

“Najaribu kubaki kushawishika na ubora wa huu mradi, Lakini nakubali na maanisha, sifikiri kama huu mradi (Europe Super League) utaendelea,” alisema kiongozi huyo.

Baada ya kutangazwa kutaka kuanzishwa kwa michuano hiyo mipya barani Ulaya ambayo ilipangwa kuchezwa katikati ya wiki mashabiki na wadau wengi wameonekana kutokubaliana na jambo hilo na kusema kuwa michuano hiyo haina afya kwa soka bali wamiliki wa klabu hizo wanaangalia fedha kulino mapenzi na mchezo husika.

Kabla ya michuano hiyo kuanza tayari benki JP Morgan kutoka America ilikuwa tayari kutoa kiasi cha dola za kimarekani bilioni 5, sawa na fedha za kitanzania trillion 11.5, huku dhumuni la kuanzisha michuano hiyo ni kuziondoa klabu kwenye ukata wa kifedha mara baada ya janga la Corona.

Ukiachilia timu hizo kutoka England klabu zingine zilizokuwa kwenye mipango na michuano hiyo ni Inter Milani, AC Millan, Juventus, Real Madrid, Barcelona na Atleticol Madrid.

Michuano hiyo ilipanga kushirikisha jumla ya timu 20, huku wadau wengi wa soka waliona kuwa ni kama njama za kutaka kuififisha michuano mikongwe ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!