SERIKALI imetenga Sh. 14 Bilioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali mpya 28, ikiwepo Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyotengewa sh.500 Milioni. Anaripoti Jemima Samweli, DMC … (endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo Tarehe 20 April 2021, bungeni jijini Dodoma na Ummy Mwalimu, Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).
Ummy ametoa kauli hiyo baada ya Jonas Mbinga, Mbunge Mbinga Vijijini kuiomba serikali ieleze, lini itaanza kujenga na kukarabati majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Mbinga kutokana na kukosa baadhi ya majengo kwani yaliyopo, yamechakaa.
“Serikali inatambua uchakavu wa baadhi ya hospitali kongwe za halmashauri ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.
“Kwa kuzingatia hali hiyo, serikali imeona ni vema katika mwaka wa fedha 2021/22 kutenga na kuomba kuidhinisha Sh.14 Bilioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa mpya wa hospitali 28, ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyotengewa Sh.500 Milioni,” amesema.
Waziri huyo pia amesema, serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kukarabati na kujenga hospitali mpya nchini, kwa awamu kadri ya upatikanaji wa fedha,” amesema.
Leave a comment