Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi
Habari Mchanganyiko

Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi

Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani
Spread the love

 

KERO ya kujaa maji eneo la Jangwani, Dar es Salaam ambapo husababisha adha kubwa ya usafiri kwa wananchi, ipo mbioni ‘kutibiwa.’ Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Serikali imesema, ipo katika mchakato wa kujenga tuta kubwa katika eneo hilo ili kuondoa kabisa kero hiyo iliyotesa wananchi kwa muda mrefu pale mvua zinaponyesha.

Kauli hiyo imetolewa na David Silinde, Naibu Waziri wa Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), leo Jumanne tarehe 13 Aprili 2021, bungeni mjini Dodoma.

Silinde alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Agnes Kaiza aliyehoji, ni lini serikali itamaliza kero ya wananchi wa Dar es Salaam hasa eneo la Jangwani?

“Serikali imeweka mkakati wa kumaliza kero hiyo kwa kujenga miundombinu itakayopitisha maji ili yasituame na kuwa kero,” amesema.

Amesema, serikali inatengeneza mkakati maalumu wa kuhakikisha inajenga miundombinu imara ya kuondoa matatizo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!