Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi
Habari Mchanganyiko

Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi

Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani
Spread the love

 

KERO ya kujaa maji eneo la Jangwani, Dar es Salaam ambapo husababisha adha kubwa ya usafiri kwa wananchi, ipo mbioni ‘kutibiwa.’ Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Serikali imesema, ipo katika mchakato wa kujenga tuta kubwa katika eneo hilo ili kuondoa kabisa kero hiyo iliyotesa wananchi kwa muda mrefu pale mvua zinaponyesha.

Kauli hiyo imetolewa na David Silinde, Naibu Waziri wa Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), leo Jumanne tarehe 13 Aprili 2021, bungeni mjini Dodoma.

Silinde alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Agnes Kaiza aliyehoji, ni lini serikali itamaliza kero ya wananchi wa Dar es Salaam hasa eneo la Jangwani?

“Serikali imeweka mkakati wa kumaliza kero hiyo kwa kujenga miundombinu itakayopitisha maji ili yasituame na kuwa kero,” amesema.

Amesema, serikali inatengeneza mkakati maalumu wa kuhakikisha inajenga miundombinu imara ya kuondoa matatizo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!