Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi
Habari Mchanganyiko

Kero Jangwani, Dar kumalizwa hivi

Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani
Spread the love

 

KERO ya kujaa maji eneo la Jangwani, Dar es Salaam ambapo husababisha adha kubwa ya usafiri kwa wananchi, ipo mbioni ‘kutibiwa.’ Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Serikali imesema, ipo katika mchakato wa kujenga tuta kubwa katika eneo hilo ili kuondoa kabisa kero hiyo iliyotesa wananchi kwa muda mrefu pale mvua zinaponyesha.

Kauli hiyo imetolewa na David Silinde, Naibu Waziri wa Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), leo Jumanne tarehe 13 Aprili 2021, bungeni mjini Dodoma.

Silinde alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Agnes Kaiza aliyehoji, ni lini serikali itamaliza kero ya wananchi wa Dar es Salaam hasa eneo la Jangwani?

“Serikali imeweka mkakati wa kumaliza kero hiyo kwa kujenga miundombinu itakayopitisha maji ili yasituame na kuwa kero,” amesema.

Amesema, serikali inatengeneza mkakati maalumu wa kuhakikisha inajenga miundombinu imara ya kuondoa matatizo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!