Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndege tatu mpya kutua nchini
Habari za Siasa

Ndege tatu mpya kutua nchini

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Spread the love

 

NDEGE tatu zitatua nchini muda wowote baada ya Serikali ya Tanzania, kukamilisha malipo ya ununuzi wa ndege hizo tatu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Katika ndege hizo tatu, mbili ni Airbus A220-300 na moja ni Dash 8-Q400De-Havilland. Ndege hizo zinatarajiwa kuwasili kati ya 2021 na 2022.

Kuwasili kwa ndege hizo, kutafanya jumla ya ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kuwa jumla ya ndege  12.

Kauli ya ununuzi wa ndege hizo imetolewa leo tarehe 13 Aprili 2021, bungeni mjini Dodoma na Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wakati akiwasilisha mwelekezo wa kazi za serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2021/22.

“Nitumie fursa hii kulipongeza Shirika la Ndege Tanzania    kwa    kuanzisha safari za kwenda Guangzhou, China,” amesema Waziri Majaliwa.

1 Comment

  • Hao wasafiri wa Guangzu ni kina nani? Watanzania wanaruhusiwa kuingia huko bila ya chanjo na barakoa? Au watasema wao wanalindwa na kupendelewa na Mungu?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!