Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mamilioni yapigwa kituo mabasi mwendokasi – CAG
Habari za Siasa

Mamilioni yapigwa kituo mabasi mwendokasi – CAG

Spread the love

 

RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2019/2020, imebaini kituo cha mabasi cha yaendayo haraka cha Kariakoo, jijini Dar es Salaam, kujengwa tofauti na mchoro ulivyooneshwa. Anaripoti Matilda Peter, Dar es Salaam … (endelea).

Ripoti hiyo iliyoandaliwa na CAG, Charles Kichere imewasilishwa bungeni jana Alhamisi, tarehe 8 Aprili 2021.

Kichere amesema katika uchunguzi wake kwenye mradi huo”nilibaini kituo cha mabasi cha Kariakoo kutojengwa kama mchoro ulivyoonesha kwa kujenga fremu ya aina tofauti na iliyoidhinishwa.”

Amesema, hatua hiyo “imesababisha malipo ya ziada ya Sh.234.37 milioni. Baada ya kuhoji uhalali wa malipo ya ziada, mshauri elekezi alirudisha Sh.130.89 milion, kama sehemu ya malipo yaliyozidi na kuacha kiasi cha Sh.103.48 milioni ambacho hakijarejeshwa.”

“Aidha, nilibaini nguzo zilizojengwa kwenye kituo hicho, zilikuwa fupi kuliko kimo kilichotakiwa kwenye michoro ya usanifu na michoro ya kina na kusababisha malipo ya ziada ya Sh.91.14 milioni,” amesema

Amesema, baada ya ukaguzi huo, Sh.83.43 milioni kati ya Sh.91.14 milioni, zilirejeshwa na mkandarasi na kuacha kiasi cha Sh.7.71 milioni ambacho hakikurejeshwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!