Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Miradi ya uwekezaji yapungua kwa miaka mitano- CAG
Habari za Siasa

Miradi ya uwekezaji yapungua kwa miaka mitano- CAG

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)
Spread the love

 

CHARLES Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amesema miradi mipya inayosajiliwa katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), imepungua kwa asilimia 48, katika kipindi cha miaka mitano mfululizo (2015/16 hadi 2019/20). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

CAG Kichere ametoa taarifa hiyo leo Alhamisi tarehe 8 Aprili 2021, wakati anatoa muhtasari wa taarifa ya ukaguzi kwa mwaka 2019/2020, jijini Dodoma.

“Katika mapitio yangu ya taarifa za mwaka na kanzi data ya wawekezaji katika TIC, nilibaini kushuka kwa idadi ya miradi inayosajiliwa na TIC, kwenye kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2015/16 mpaka mwaka 2019/20,” amesema CAG Kichere.

Mkaguzi huyo wa hesabu za Serikali amesema, miradi hiyo imepungua kutoka 420 iliyosajiliwa TIC mwaka 2015/16 hadi kufikia 219 mwaka 2019/2020.

Wakati huo huo, CAG Kichere amesema, katika kipindi hiko, kiasi cha mitaji na nafasi za kazi zinazotokana na uwekezezaji, zilishuka.

“Pamoja na kushuka kwa idadi ya miradi, pia nilibaini kushuka kwa kiasi cha mitaji pamoja na idadi ya nafasi za kazi zinazotokana na uwekezaji,” amesema CAG Kichere.

CAG Kichere amesema, changamoto hizo zimesababishwa na mabadiliko ya Sheria ya Fedha ya 2015, ambayo iliondoa baadhi ya vivutio vya kodi kwa wawekezaji.

“Kupungua kwa idadi ya miradi mipya pamoja na mambo mengine, kunatokana na mabadiliko ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2015 ambayo iliondoa baadhi ya vivutio vya kodi kwa wawekezaji.”

“Kwa mfano kuondoa vivutio vya kodi katika upanuzi wa miradi kutoka katika kundi la miradi inayopaswa kupewa vivutio vya kodi,” amesema CAG Kichere.

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

Amesema kushuka kwa idadi ya uwekezaji kuna athari kubwa kwa Taifa, kwani kunapunguza fursa ya ajira, kodi, ujuzi pamoja na usambazaji wa Teknolojia.

Taarifa hiyo ya CAG Kichere imekuja siku mbili tangu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuiagiza Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, kuboresha mazingira ya uwekezaji.

Akizungumza katika hafla ya uapisho wa viongozi katika Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 6 Aprili 2021, Rais Samia aliagiza wizara hiyo iboreshe taratibu za utoaji vibali na viwango vya utozaji kodi, ili kuwavutia wawekezaji wapya na waliokimbia nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!