Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwigulu ataja sababu ongezeko deni la Taifa
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mwigulu ataja sababu ongezeko deni la Taifa

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba, ametoa sababu ya kuongezeka kwa deni la taifa, kutoka Sh.54.8 trilioni mwaka 2019 hadi Sh.59 trilioni mwaka 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amesema, ongezeko hilo ni sawa na asilimia 7.6.

Dk. Mwigulu amesema hayo leo Alhamisi, tarehe 8 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha mapendekezo ya serikali ya mpango wa maendeleo ya taifa na kiwango cha ukomo wa bajeti ya serikali kwa mwaka 2021/22.

Waziri huyo amesema, kati ya kiasi hicho, deni la nje ni Sh.42.8 trilioni 42.8 na deni la ndani Sh.16.2 trilioni.

Akielezea sababu zilizochagiza kuendezeka, Dk. Mwigulu amesema “kupokelewa kwa fedha za mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, umeme na maji.”

“Na malimbikizo ya riba ya deni la nje, hususan nchi zisizo wanachama wa kundi la Paris Club ambazo Serikali inaendelea kujadiliana nazo.”

“Aidha, matokeo ya tathmini ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Desemba 2020 yanaonesha kuwa deni ni himilivu kwa muda mfupi, wa kati na mrefu,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!