Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Mwigulu: Rais anaimani na wana Yanga
Michezo

Mwigulu: Rais anaimani na wana Yanga

Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba amesema kuwa kuteuliwa kwake kuwa waziri wa wizara hiyo pamoja na uteuzi wa Makamu wa Rais, Dk. Philipo Mpango kunaonesha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaimani kubwa na wana Yanga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mwigulu ameyasema hayo hii leo tarehe 8 Machi, 2021, Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiwasilisha mpango wa tatu wa maendeleo.

Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Katika maneno yake ya ufunguzi wakati wa hotuba hiyo, Mwigulu ambaye ni shabiki wa klabu ya Yanga alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteuwa kwenye nafasi hiyo pamoja na kumteua Dk. Philip Mpango na hivyo kuonesha imani kubwa kwa mashabiki hao wa Yanga.

“Mheshimiwa Spika kwa kipekee napenda kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuniamini na kuniteuwa kuwa Waziri wa Fedha, kwa uteuzi wangu na uteuzi wa Makamu wa Rais, Dk. Mpango inaonesha rais anaimani kubwa na wana Yanga,” alisema.

Dk Philip Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mwigulu aliteuliwa tarehe 31 Machi, 2021 na Rais Samia kuwa Waziri wa Fedha na Mipango akitokea Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa hafla ya kumuapisha Makamu wa Rais, Dk. Mpango.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!