Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Balozi wa Italia auawa DRC
Kimataifa

Balozi wa Italia auawa DRC

Luca Attanasio
Spread the love

 

LUCA Attanasio, Balozi wa Italia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ameuawa katika shambulio lililolenga magari ya Umoja wa Mataifa (UN). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Luigi Di Maio, Waziri ya Mambo ya Nje ya Italia ameeleza, balozi wake ameuawa jana tarehe 22 Februari 2021, sambamba na mwanajeshi wa taifa hilo baada ya msafara kushambuliwa na waasi.

“Kwa masikitiko makubwa, wizara ya mashauri ya kigeni inathibitisha kifo cha balozi kilichotokea jana, mjini Goma,” taarifa ya wizara imesema.

Sambamba na vifo hivyo, dereva mmoja raia wa DRC naye aliuawa. shambulio hilo lilitokea karibu na Mji wa Kanyamahoro uliopo Mashariki mwa nchi hiyo.

Taarifa zaidi zinaeleza, lengo la waasi kufanya shambuli hilo, lililenga kuteka nyara, makundi hayo yamekuwa yakitumia Mbuga ya Wanyama ya Virunga kutekeleza uasi huo.

Mbuga hiyo inapakana na Rwanda na Uganda ambapo walinzi wake wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara na hata kuuawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!