Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Balozi wa Italia auawa DRC
Kimataifa

Balozi wa Italia auawa DRC

Luca Attanasio
Spread the love

 

LUCA Attanasio, Balozi wa Italia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ameuawa katika shambulio lililolenga magari ya Umoja wa Mataifa (UN). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Luigi Di Maio, Waziri ya Mambo ya Nje ya Italia ameeleza, balozi wake ameuawa jana tarehe 22 Februari 2021, sambamba na mwanajeshi wa taifa hilo baada ya msafara kushambuliwa na waasi.

“Kwa masikitiko makubwa, wizara ya mashauri ya kigeni inathibitisha kifo cha balozi kilichotokea jana, mjini Goma,” taarifa ya wizara imesema.

Sambamba na vifo hivyo, dereva mmoja raia wa DRC naye aliuawa. shambulio hilo lilitokea karibu na Mji wa Kanyamahoro uliopo Mashariki mwa nchi hiyo.

Taarifa zaidi zinaeleza, lengo la waasi kufanya shambuli hilo, lililenga kuteka nyara, makundi hayo yamekuwa yakitumia Mbuga ya Wanyama ya Virunga kutekeleza uasi huo.

Mbuga hiyo inapakana na Rwanda na Uganda ambapo walinzi wake wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara na hata kuuawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!