Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Balozi wa Italia auawa DRC
Kimataifa

Balozi wa Italia auawa DRC

Luca Attanasio
Spread the love

 

LUCA Attanasio, Balozi wa Italia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ameuawa katika shambulio lililolenga magari ya Umoja wa Mataifa (UN). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Luigi Di Maio, Waziri ya Mambo ya Nje ya Italia ameeleza, balozi wake ameuawa jana tarehe 22 Februari 2021, sambamba na mwanajeshi wa taifa hilo baada ya msafara kushambuliwa na waasi.

“Kwa masikitiko makubwa, wizara ya mashauri ya kigeni inathibitisha kifo cha balozi kilichotokea jana, mjini Goma,” taarifa ya wizara imesema.

Sambamba na vifo hivyo, dereva mmoja raia wa DRC naye aliuawa. shambulio hilo lilitokea karibu na Mji wa Kanyamahoro uliopo Mashariki mwa nchi hiyo.

Taarifa zaidi zinaeleza, lengo la waasi kufanya shambuli hilo, lililenga kuteka nyara, makundi hayo yamekuwa yakitumia Mbuga ya Wanyama ya Virunga kutekeleza uasi huo.

Mbuga hiyo inapakana na Rwanda na Uganda ambapo walinzi wake wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara na hata kuuawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mpinzani mkuu wa Rais Kagame aachiwa huru

Spread the love  PAUL Rusesabagina, aliyewahi kuripotiwa kama ‘shujaa’ katika filamu ya...

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

error: Content is protected !!